27 July 2024 00:00:00 AM Trending Posts
Cleaning is no dirty business for entrepreneur Agnes KipaloMagufuli to attend Kenyatta’s swearing-in ceremony Davido Releases a New Record, "Like Dat"Zimbabwe: President to Hit Ground RunningNigeria: Ahead of Afrima 2017, Organizers Unveil Akon, Sophy Aiida As HostsTanzania: Turnout Excites Dar Tourism Expo OrganizersTanzania: All About Diamond's WomenTanzania: Here is Diamond's Hot Tune Featuring Morgan HeritageTanzania: Business Opportunities With Tanzania to Be IncreasedTanzania: Business Opportunities With Tanzania to Be IncreasedTanzania: Boost for Tanzania Cassava As Chinese Firm to Invest $1 BillionTanzania: Diamond Platnumz - Yes, I Cheated On ZariTanzania: Diamond, Zari in Fresh 'Cheating' StormNape Aeleza Kwanini Dr Kikwete Hakutengeneza Uadui Na WapinzaniBaraza la Maaskofu Katoliki Tanzania watoa tamko kushambuliwa kwa Mhe. LissuTanzania: Better Services Beckon As Digitized Systems Kick OffSouth Africa: BRICS is Being Battered by Global Crises - Why This Might Not Be a Bad ThingTanzania Girls' Monthly Nightmare Force Them Out of ClassesTanzania: Scientists Find Fossils of Rare Dinosaur in TanzaniaCourt Ready to Deliver Kenya's Presidential Petition RulingTanzania: Ali Kiba and Nandy Nominated for Afrima AwardsTanzania proposes higher petroleum levy to fund budgetZanzibar in short supply of skilled tourism staffAfrican Airlines Wait for Open SkiesDrone Project Will Deliver Medicines Across TanzaniaTanzania: Diamond Platinumz Caught in Claims of Fathering Model's Baby

Nape Aeleza Kwanini Dr Kikwete Hakutengeneza Uadui Na Wapinzani

Mbunge wa jimbo la Mtama kupitia tiketi ya CCM, Nape Nnauye amefafanua kauli yake ya kuiunga mkono kauli ya Rais mstaafu, Dr Jakaya Kikwete na kuwataka viongozi waafrika waache kuwachukulia wapinzani wa vyama vya siasa kama maaduzi zao

Mbunge wa jimbo la Mtama kupitia tiketi ya CCM, Nape Nnauye amefafanua kauli yake ya kuiunga mkono kauli ya Rais mstaafu, Dr Jakaya Kikwete na kuwataka viongozi waafrika waache kuwachukulia wapinzani wa vyama vya siasa kama maaduzi zao.

Akiongea katika mahojiano maalumu na Bongo5 wiki hii mkoani Dodoma, Nape amesema siasa isiwafanye watu wakaanza kuchukiana na kujengeana chiki.

“Nilikomenti kupitia mitandao ya kijamii, nilisema mimi namuunga mkono Dr Jakaya. Wapinzani sio maadui, mimi nakaa nao napika nao chakula tunakula. Upinzani sio uadui, ni wadau katika kuendesha nchi, ndio maana mimi ishu ya Lissu nimepiga naye picha muda mchache kabla ya kupatwa na tukio, wapinzani wote mimi ni rafiki zangu na katika watu ambao wamefanya siasa za kupambana mimi ni mmoja wapo,” alisema Nape.

Aliongeza, “Wapinzani tuwachukulie kama ni washirika wetu, hakuna siku watatuunga mkono, lakini watatukosoa na tukiweka dhana hiyo hakuna siku tutawekeana vinyongo, halafu wakati mwingine sisi tunagombana wao wakubwa wanakaa meza moja wanakunywa chai, isifike mahali tukawekeana vinyongo tukataka kutoana roho, kwahiyo kimsingi namuunga mkono Dr Kikwete na yeye aliendesha nchi kwa ustarabu huo, anakunywa nao chai, kwanini hakuwachukulia kama maadui. Yapo mambo Kikwete aliyafanya wakati wake hata sisi wakati mwingine ndani ya CCM tulikuwa tunachukia, unakuta mahali mmembana mtu halafu yeye anafika anasema muacheni, leo tunasema tulikuwa tunasikitika lakini nadhani alikuwa anafanya sawa sio maadui zetu hawa,”